Jumatatu, 30 Machi 2020

KUCH-KUCH HOTAHE: MAKOSA AMBAYO HAUKUTAMBUA

Mwaka 1998 kanda ya Kuch Kuch Hota Hai’ rasmi ilikuwa imetoka kwa nchini India, ni kanda inayohusu mapenzi, vichekesho. Iliandikwa na Karan Johar, ni miongoni mwa kanda ambazo ziliwakutanisha watu maarufu Shah Rukh Khan na Kajol katika kanda yao ya nne kuigiza pamoja.Pia mwanadada Rani Mukerji alitokea kwenye movie akiwa kama muhusika msaidizi, na Salman Khan alikuwepo katika special appearance. Filam hii mpaka leo hii imekuwa maarufu katika televishion mbali mbali za nchini India kwa nyimbo  zake kama Koi Mil Gaya na ile ambayo imechukua jina la kanda Kuch Kuch Hot Hair, n kufikia hatua ya filamu kuwa cult classic status. Tote sawa lakini makala hii fupi imekuja kukuangazia baadhi ya makosa ambayo yalikuwa katika filamu hiyo na huenda hakuweza kuona.
1. Rani Mukherjee (Tina) alimpa barua nane mtoto wake
KKHH
Rani mukherjee (Tina) alimpatia barua 8 binti yake. Ambapo tunaambiwa kuwa kila kwenye Birthday yake alikuwa anasoma barua moja, Kwenye movie tunaonyeshwa anasoma barua ya nane kwenye katika birthday yake, Kwa kawaida ina maana kuwa huyu mtoto alikuwa anasoma barua ya kwanza akiwa na mwaka mmoja ya pili na miaka miwili nakuendelea, Je mtoto wa mwaka mmoja au miwili anaweza kusoma?

2. Eneo la Basketball
KKHH-mistake1
PICHA YA KWANZA ENEO LILIKUWA PEMBENI LINA MAUA LAKINI BAADAE ILIONYESHWA KUWA KUNA MAJI.
Katika scene ya kwanza, Unaweza ukaona kuwa upande wote wa uwanja kuna nyasi lakini katika scene nyingine inaonyesha pembeni mwa uwanja wa Basketball kuna waterbody.

3. Mtoto alitokea wapi hapa?
KKHH0
PICHA YA JUU INAONYESHA KUWA SHAH RUKH KHAN HANA MTOTO KATIKA MAGOTI YAKE LAKINI BAADAE TULIONYESHWA MTOTO WA KIKE
Wakati Kajol anacheza ‘Dumb charade’ kuna fununu walikuwa wanaulizana kuhusu mchezo huo, na katika magoti ya mtaalamu shah rurh khan kulikuwa hakuna mtu, Lakini baadae ghafla tunaona kuna mtoto wa kike ana anamshikilia huku akitoa taarifa kuhusu swali waliokuwa wanajiuliza kuhusu Dumb Charade. Swali kuwa ni wapi huyu mtoto alitokea na ana uhusiano gani na mtaalamu?

4. Shahrukh alitokea wapi?
KKHH1-1
PICHA YA JUU INAONYESHA KWENYE SEHEMU YA MAONYESHO KWENYE DUARA NYEKUNDU HAKUNA MTU LAKINI KWENYE POINT YA HILO DUARA ALITOKEA SRK ANGALIA PICHA YA CHINI YAKE
Angalia hizo scene mbili tofauti tuanze na kuichambua scene ya kwanza nyuma ya hao vijana kulikuwa hakuna mtu yeyote, Angalia alama nyekundu. Lakini baadae ghafla SRK alitokea katika eneo hilo swali alitokea wapi?.

5.Shahrukh anatembea vipi?
KKHH-mistake3
Wakati SRK anamuaga Anjali katika scene ya kwanza alikuwa yuko mbali na jukwaa angalia picha ya kwanza, Lakini baadae scene inatuonyesha kuwa amesimama katika hilo jukwaa na nyuma yake kuna Tina. Kiuharisia ni wapi SRK alisimama?

6. Stage limejisafisha lenyewe, Woow Inashangaza kwa kweli
KKHH4
Kwenye shoo ya ST. XAVIER College, Rahul (SRK) na Kajol (Anjali) waliimba vibaya wakasawazishwa, lakini watu walichukia na kuanza kuwatupia nyanya zilizooza.  Lakini dakika chache baadae Anjali, Rahul na Tina wakaanza kuimba nyimbo ya ‘Koi Mil Gaya’, kimiujiza jukwaa/stage lilionekana limejisafisha lenyewe kimiujiza.
NOTE;POST WILL BE UPDATED

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni